Naibu mwenyekiti wa tume ya uchabuzi Burundi Spes-Caritas Ndironkeye
Naibu mwenyekiti wa Tume huru ya Uchaguzi nchini Burundi Spes-Caritas
Ndironkeye ameandika barua ya kujiuzulu wadhifa huo na kuikimbia nchi
hiyo kwasababu ambazo hazijajulikana.Pia taarifa ambayo bado haijathibitishwa, inasema kuwa mkurugenzi wa masuala ya utawala na fedha kwenye Tume huru ya Uchaguzi Illuminata Ndabahagamye huenda naye amejiuzulu kwenye wadhifa huo kutokana na kushindwa kuwepo kwa maelewano mazuri na serikali ya rais Pierre Nkurunziza.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment