Zaidi ya watu 35 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 55 wamejeruhiwa
baada ya nyumba zao kuwaangukia na kuwafunika usiku wa kuamkia leo
kutokana na mvua kubwa iliyonyesha wilayani Kahama, mkoani Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya
Taarifa zilizothibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya
amesema mvua hiyo kubwa iliambatana na upepo mkali, hivyo nyumba nyingi
zilianguka na nyingine kuezuliwa na kuharibiwa kabisa.
Bw. Mpesya amesema hadi majira ya asubuhi walikuwa wamefanikiwa
kupata miili ya watu 35 waliopoteza maisha baada ya kufukua nyumba
nyingi, na majeruhi wamekimbizwa hospitali ya wilaya kwa matibabu.
Mkuu huyo wa Wilaya amesema nyumba nyingi zimeanguka na zoezi la kutafuta watu waliojeruhiwa au kupoteza maisha bado linaendelea kwa kasi.
Mkuu huyo wa Wilaya amesema nyumba nyingi zimeanguka na zoezi la kutafuta watu waliojeruhiwa au kupoteza maisha bado linaendelea kwa kasi.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment