STAA
wa Bongo Fleva,Rehema Chalamila’’Ray C’ ameahirisha kuisambaza ngoma
yake kwenye vituo vya redio kupisha msiba wa rafiki yake wa siku nyingi
marehemu Aisha Madinda,ngoma hiyo inaitwa Nishum Shum tayari ipo kwenye
mitandao.
Kupitia Instagram Ray C aliandika hivi...Nenda Dada yangu nenda!
Nakumbuka tulikutana Kanisani Tabata ukanishuhudia Kwamba umeweza kuacha
madawa ya kulevya na miguu yako imepona Kabisa kwa imani na mola na kwa
maombezi ya nabii Joseph, nilipokuona ulivyokuwa umependeza nikajipa
moyo huku nalia kwamba iko siku na mimi nitaacha madawa tulilia sana
mimi na mama yangu pale Kanisani huku tukimwomba mungu aniokoe kwenye
mateso yale, uliniangalia kwa huruMa wakati mimi na mama tunaondoka pale
Kanisani ukamkimbilia mama na kumwomba namba yake huku ukimuahidi kuwa
nitapona tu........Siku niliokutana na wewe tena mwananyamala hospitali
ulinipita bila kunitambua nikakuita aisha? Ray C hapa ! Hukuamini macho
yako kutakana na nilivyokuwa nimenenepa, tulicheka kwa furaha
tukakumbushiana ya kanisani ukaniambia si nilikwambia utapona kwa uwezo
wa mungu??? Nikamwambia natibiwa na methadone na wewe pia uko kitengo
hichohicho muhimbili, tukaagana kwani nilikuwa nawahi kunywa dawa
TUKAAGANA! NDIO SIKU YA MWISHO KUKUONA!Dada angu tangulia uniwekee na
nafasi kwani najua lazma tutakuja onana tena mbele, ya haki, nimeshtuka
sana ila najua mungu yuko nawe my sister, I will aways remember You
DEAR.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment