November 20, 2014


 
Ni stori nyingi tunakutana nazo kwenye vyombo vya habari kila tunapoamka na mara nyingi tunaamka nazo kwenye mitandao ya kijamii moja wapo ikiwa hii ya mwimbaji wa Uganda Jose Chameleone kudaiwa kumuomba Diamond wafanye collabo. Kwenye interview na Mambo Mseto ya Radio Citizen November 19 2014 Chameleone amekanusha hizo taarifa kwa kusema ‘kitu ambacho nitakwambia kabla ya kusema chochote, mimi naheshimu wasanii wote mashariki na duniani na nataka niwakumbushe kitu kingine, nimekaa kwenye muziki kwa miaka kumi na nne… mimi sio msanii mchanga’ 

‘Ilikua ni uongo sijui umetokea wapi eti mimi nimemuomba collabo, Yes…. tunaweza kufanya collabo lakini mimi sijamuomba collabo, wamesema mimi nimezungumza na Diamond kwenye whatsapp… yes tumezungumza lakini ilikua ni kirafiki wala hatujaongea maneno ya kimuziki’ – Jose 

‘Mimi ni msanii mkubwa, sio msanii mchanga… naheshimu kila msanii kuanzia mchanga mpaka mkubwa na vilevile mimi pia ni msanii mkubwa na siwezi kuomba collabo kama hivyo, nimeshangazwa sana’

MSIKILIZE HAPA

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE