October 23, 2014

Sakata la umri la Miss Tanzania 2014 Sitti Mtevu limeendelea kuchukua sura mpya baada ya Baraza la Sanaa Taifa (Basata) kudai kuwa litamvua taji hilo endapo watagundua kasoro za umri zinazodaiwa
Akizungumza na gazeti la Nipashe, Katibu Mkuu wa Basata, Geoffrey Mwingereza , alisema wanasubiri uchunguzi wao ukamilike na wakibaidi udanganyifu watamvua taji hilo. 
Wakati Mwingereza akielezea taarifa hiyo, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wanatarajia kukutana leo jijini Dar es salaam kwajili ya kujadili sakata hilo. 
Akizungumza na gazeti hilo jana, Naibu Waziri wa Wizara ya Michezo, Juma Nkamia alisema serikali imelisikia sakata la mrembo huyo na wameamua kuitisha kikao ili kulifanyia kazi. 
"Siwezi kukuambia hatua gani zitachuliwa, ila kesho, (leo) tutakuwa na kikao , serekali haiwezi kukaa kimya , kuna vyombo vyake vinalifanyia kazi" alisema Nkamia. 
Aliongeza kuwa yeye alikuwa nje ya Dar es Salaam lakini kuna maelezo aliyoyatoa na yameanza kufanyiwa kaz

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE