Nabii maarufu ndani na nje ya
bara la Afrika TB Joshua wa
kanisa la All nations (Scoan) la
nchini Nigeria ametuma chupa
4000 za maji ya upako pamoja na
dola za kimarekani 50,000 nchini
Sierra Leon ili kusaidia kutibu
ugonjwa wa ebola ambao
umeikamata nchi hiyo.
Nabii Joshua amesema kupitia
tovuti ya kanisa lake kwamba
maji hayo yamesafirishwa kwa
ndege maalumu ya kukodi
ambayo gharama yake pia ni
dola 50,000 na kufanya gharama
kamili dola 100,000 (laki moja)
kwa msaada alioutoa
akishirikiana na wadau wa
Emanuel TV ya kanisa lake.
Katika taarifa yake kupitia tovuti
hiyo nabii TB Joshua amesema
Mungu mwenye nguvu
atajidhihirisha uweza wake
kupitia maji hayo ya upako
ambayo yametolewa kwa watu
waliokumbwa na ebola. "Sio maji
ndiyo ya ponyayo wagonjwa ila ni
Yesu mwenyewe, lazima mtu
anayemuombea mwingine na
yule anayeombewa wawe na
imani. lazima imani iwe hai ili
kupata uponyaji kwasababu ndiyo
husababisha uponyaji na sio maji
ya upako" amekaririwa nabii
Joshua.
Watu waliotumia maji hayo ya
upako wamekiri kuwa na imani
nayo kutokana na wengi
kufunguliwa na miujiza mingi
kutendeka kutoka hali ya
kutokuwa na uwezo wa kuzaa na
hatimaye kupata mtoto lakini pia
maji hayo yamekuwa kinga ya
risasi kupenya kwenye gari kama
mtu mmoja kutoka nchini Ghana
alivyopona mikononi mwa
majambazi waliokuwa
wakishambulia kwa risasi gari
lake yeye akiwemo ndani bila
mafanikio. Na mdadisiblog/festosaimon |
0 MAONI YAKO:
Post a Comment