August 21, 2014

 
Stori:Chande Abdallah na Deogratius Mongela
Inaumiza kusikia! Watoto watatu ambao ni majirani wamejikuta wakiingia kwenye kadhia ya kubakwa kwa zamu na watoto wenzao ambapo mmoja anadaiwa kuwa na umri wa miaka 17 huku mwingine akiwa na umri wa miaka 14 ambaye pia ni denti wa darasa la nne.
 
Watoto watatu wadogo waliobakwa kwa zamu na watoto wenzao.
Tukio hilo la aina yake lilijiri hivi karibuni maeneo ya Mbagala-Mianzini jijini Dar ambapo awali ilidaiwa kuwa wazazi wa watoto hao walishtushwa walipogundua watoto wao wameingiliwa na kuharibika vibaya baada ya kuwakagua kila mmoja kwa wakati wake walipokuwa wakiwaogesha.
 
Wazazi wa kiume wa watoto hao.
Wakizungumza na gazeti hili kwa masikitiko kwa nyakati tofauti, wazazi wa watoto hao walidai kwamba walipowabana waliwataja kwa majina waliowafanyia vitendo hivyo, jambo lililowafanya ‘kuwataiti’ watuhumiwa kwani walikuwa wakiwafahamu.
Wazazi hao walidai kwamba walipowauliza watoto hao walikiri kuwaingilia wenzao kwa zamu kwenye jumba bovu (pagala) ambapo walienda mbali zaidi na kusema kuwa walikuwa wamewafanyia vitendo hivyo kwa muda mrefu sasa kwa zamu, nyakati ambazo watoto hao walirejea kutoka shuleni chekechea (jina kapuni kimaadili).
 
Wazazi wa kike wa watoto hao.
“Nilishtuka na kuumia sana baada ya kugundua mwanangu ameingiliwa, tena kwa kipindi kirefu kiasi kwamba ameharibika kabisa.
“Huwezi kuamini mke wangu alipopata taarifa alipandwa na presha kiasi cha maisha yake kuwa hatarini,” alisema mmoja wa wazazi hao aliyejitambulisha kwa jina moja la Hussein.
 
Waraka(RB) wa polisi wa kukamatwa kwa watuhumiwa.
Kwa pamoja wazazi hao waliripoti ishu hiyo kwenye Kituo cha Polisi cha Charambe na baadaye Mbagala-Kizuiani ambapo majalada ya kesi hizo yalisomeka MBL/RB/9608/14-KUBAKA, CHAR/RB/1292/2014-KUBAKA CHAR/RB/2192/2014-KUBAKA ambapo watuhumiwa wanasubiri kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Chanzo:globalpublishers.info

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE