August 21, 2014

 
Na Imelda Mtema
STAA wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja, ameibuka na kudai kuwa ameweka vitu vyote vya kitoto pembeni likiwemo suala la malumbano na kujikita katika suala la ujasiriamali.
 
Staa wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja.
Akizungumza na paparazi wetu, Kajala alisema amefanya tathmini na kugundua mastaa wengi wamekuwa wakiambulia umaskini baada ya umaarufu kupotea hivyo ameona ashtuke mapema kwa kufanya biashara mbalimbali ambazo zitamjengea msingi mzuri maishani.
 
Staa wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu.
“Nimeshtuka, sihitaji bifu na mtu, biashara tu na hata safari za nchini China kwa sasa ni kwa ajili ya biashara pekee na si vinginevyo, ukitaka pochi, viatu na vitu vingine vingi utapata,” alisema Kajala aliyekuwa akiogelea katika bifu kali na aliyekuwa shosti wake, Wema Sepetu.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE