Rais
wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya mrisho kikwete leo
amepokea Tuzo ya Kiongozi Bora wa Maendeleo Afrika tuzo ambayo hutolewa
na Taasisi inayochapisha Gazeti la African Leadership la nchini
Marekani.
Akikabidhi tuzo hiyo Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa
Kimataifa Benard Membe ambaye aliipokea tuzo hiyo nchini Marekani kwa
niaba ya Rais Kikwete amesema kutunukiwa kwa tuzo hiyo kulitokana na
kushindanishwa katika vigezo mbali mbali.
Wasomaji wa gazeti hilo walimchagua Rais Kikwete kwa zaidi ya kura
laki nne ambazo ndizo zilizomfanya kuwa mshindi kwa mwaka uliopita wa
2013.
Aidha amesema miongoni mwa sifa zilizomwezesha Rais KIKWETE kutwaa
tuzo hiyo ni pamoja na kuiendeleza nchi kiuchumi, pamoja na kukuza
maendeleo ya watu,Akiipokea tuzo hiyo kwa furaha kubwa Rais KIKWETE
amesema, ni ya watanzania wote.
Rais Kikwete amekuwa kiongozi wa tatu Afrika kupokea tuzo hiyo,
ambapo Kabla ya Rais Kikwete, tuzo hiyo ilikwishatolewa kwa marais wa
Sierra leone na Liber
0 MAONI YAKO:
Post a Comment